Visit National Business Portal for more procedures

Biashara ya Mpakani

Idara ya Ushuru na Forodha inasimamia kodi zote zinazohusu biashara ya kimataifa. Kodi hizo ni pamoja na Kodi ya Uingizaji Bidhaa, Ushuru na Kodi ya Ongezeko la Thamani kwa bidhaa ziingizwazo nchini. Kodi ya uingizaji bidhaa ni kodi inayotozwa kwa bidhaa zinazoingizwa nchini. Ushuru hukokotolewa kwa kiwango cha thamani ya kitu kwa bidhaa zilizoingizwa nchini baada ya kulipiwa bima na uchukuzi (CIF) na hukusanywa kabla bidhaa hazijaondoka kwenye kituo cha kuingilia na au kwenye mabohari-ushuru.

Ushuru
Ushuru hutozwa kwa baadhi ya bidhaa za matumizi zilizoingizwa nchini. Kimsingi bidhaa zinazotozwa ushuru ni bidhaa ambazo matumizi yake yanaonekana na jamii kuwa si ya lazima kama vile bia, sigara na bidhaa ambazo matumizi yake yanaonesha picha mbaya ya ugeni kwa jamii, kama vile petroli. Nchini Tanzania licha ya bidhaa zinazotozwa ushuru, vinywaji vya baridi na magari yanatozwa ushuru kwa madhumuni ya kupata mapato.

Inatozwa pia kwa bidhaa mahususi au kutegemea thamani halisi ya bidhaa na viwango vya kodi kwa thamani halisi ya bidhaa ni bei ya bidhaa, bima na gharama ya uchukuzi (CIF) na pamoja na ushuru wa uingizaji bidhaa.
Uingizaji Bidhaa
Kwa kawaida nchini Tanzania bidhaa zinaingizwa nchini kupitia bandari ya Dar es Salaam, Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere wa Dar es salaam na Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro. Baadhi ya bidhaa huingizwa nchini kupitia mipaka ya nchi kavu hasa inayopakana na nchi jirani. Licha ya kodi ya uingizaji bidhaa, ushuru, kodi ya ongezeko la thamani, bidhaa zinalazimika kutozwa gharama za bandari na za uwanja wa ndege.

Malipo ya kodi ya uingizaji bidhaa na ushuru zaidi ya milioni tano kwa kawaida hulipwa kupitia benki za biashara. Malipo ya kodi ya uingizaji bidhaa na ushuru chini ya shilingi milioni tano yanafanywa kupitia tawi la City Bank lililopo katika ofisi za Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kwenye Jengo la Forodha. Kabla ya kuanza mchakato wa uingizaji bidhaa waingizaji wanashauriwa kuwasiliana na Idara za serikali zinazohusika kwa ajili ya idhini kutegemea aina ya bidhaa zinazoingizwa. Idara hizo ni pamoja na Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika , Wakala ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali, Mamlaka ya Chakula na Dawa Tanzania, Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi, Wizara ya Maliasili na Utalii, Shirika la Viwango Tanzania, Tume ya Nishati ya Atomiki na Tume ya Ushindani wa Biashara.
kusafirisha bidhaa
menuPic1 menuPic2 menuPic3