Biashara ya Mpakani
Idara ya Ushuru na Forodha inasimamia kodi zote zinazohusu biashara ya kimataifa. Kodi hizo ni pamoja na Kodi ya Uingizaji Bidhaa, Ushuru na Kodi ya Ongezeko la Thamani kwa bidhaa ziingizwazo nchini. Kodi ya uingizaji bidhaa ni kodi inayotozwa kwa bidhaa zinazoingizwa nchini. Ushuru hukokotolewa kwa kiwango cha thamani ya kitu kwa bidhaa zilizoingizwa nchini baada ya kulipiwa bima na uchukuzi (CIF) na hukusanywa kabla bidhaa hazijaondoka kwenye kituo cha kuingilia na au kwenye mabohari-ushuru.
Ushuru
Ushuru hutozwa kwa baadhi ya bidhaa za matumizi zilizoingizwa nchini. Kimsingi bidhaa zinazotozwa ushuru ni bidhaa ambazo matumizi yake yanaonekana na jamii kuwa si ya lazima kama vile bia, sigara na bidhaa ambazo matumizi yake yanaonesha picha mbaya ya ugeni kwa jamii, kama vile petroli. Nchini Tanzania licha ya bidhaa zinazotozwa ushuru, vinywaji vya baridi na magari yanatozwa ushuru kwa madhumuni ya kupata mapato.
Inatozwa pia kwa bidhaa mahususi au kutegemea thamani halisi ya bidhaa na viwango vya kodi kwa thamani halisi ya bidhaa ni bei ya bidhaa, bima na gharama ya uchukuzi (CIF) na pamoja na ushuru wa uingizaji bidhaa.